Posts

Showing posts from September, 2023

KIKUNDI CHA WAVUVI KATA YA SAMAZI CHAPATA MKOPO WA BOTI NA ZANA ZA UVUVI

Image
 Wizara ya Mifugo na uvuvi kupitia Benki ya maendeleo ya kilimo Tanzania TDB imesaini Mkataba wa mkopo wa boti ya uvuvi na zana za uvuvi Kwa kikundi Cha uvuvi Cha Umoja kilichopo kata ya Samazi Wilaya ya Kalambo Mkoa wa Rukwa kama hatua yakuwawezesha wavuvi kujikwamua kiuchumi. Akiongea ofisini kwake wakati wa hafla fupi ya kusaini Mkataba huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Kalambo Shafi Mpemba,amesema mkopo huo una thamani ya Shilingi Milioni thelathini na Saba na kwamba umetolewa kwa ajili ya ununuzi wa boti aina ya Fiber,nyavu,mashine na kifaa Cha kutafutia samaki ziwani. Licha ya Hilo Mpenda aliipongeza Serikali ya awamu ya sita kupitia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa mkopo huo pamoja na boti mbili zenye thamani ya milioni 108 ambazo kwa pamoja zinaenda kusaidia kudhibiti uvuvi haramu,Udhibiti na usimamizi wa rasilimali uvuvi katika kata ya Kasanga na Samazi katika mwambao wa Ziwa Tanganyika. Kwa upande wake diwani wa kata ya

WAGANGA WAKUU WA MIKOA WAAGIZWA KUKAMILISHA MAANDALIZI YA CHANJO YA POLIO

Image
 Waganga wakuu wa Mikoa ya Rukwa ,Songwe,Katavi,Mbeya na Kagera wametakiwa kukamilisha maandalizi ya Kampeni ya kitaifa ya chanjo dhidi ya Polio inayotarajiwa kufanyika tarehe 21 hadi 24 Septemba 2023. Mganga Mkuu wa Serikali Prof.Tumain Nagu ametoa maelekezo hayo Leo tarehe 15 Septemba 2023 alipofanya kikao na watumishi wa sekta ya Afya mkoani Rukwa. Profesa Nagu ametoa maelekezo kwa waganga wakuu wa Mikoa na Wilaya zilizomo katika mikoa hiyo kukamilisha maandalizi kabla ya tarehe hizo. Amesema kuwa polio ni ugonjwa wa kuambukiza unaosababisha ulemavu wa viungo na unaoweza kusababisha kifo.Njia mojawapo ya maambukizi ni kupitia kinyesi hivyo ametaka wananchi wote wakumbushwe na kuelekezwa kuwa na vyoo Bora na kuvitumia kwa usahihi. Amewataka waganga wakuu wa Mikoa na Wilaya kuhakikisha watoto wenye umri wa miaka nane kushuka chini anafikiwa pasipo kujali changamoto za kijiografia . Amewaeleza kuhakikisha chanjo inapatikana katika maeneo yote yaliyotengwa kwa shughuli hiyo na kuhakikis

RUKWA YAPONGEZWA MAANDALIZI YA UDTHIBITI POLIO

Image
 Mganga Mkuu wa Serikali Pro.Tumain Nagu ameipongeza timu ya uendeshaji wa Huduma za Afya ngazi ya Mkoa (RHMT) ya Mkoa wa Rukwa kwa maandalizi na hatua za haraka zilizochukuliwa baada ya kisa kimoja Cha Polio kuripotiwa hapo tarehe 26 Mei ,2023. Ameyazungumza hayo Leo Septemba  14,2023 alipofanya kikao na timu ya uendeshaji wa Huduma za Afya ngazi ya Mkoa (RHMT) wakati wa kujadili na kukagua maandalizi ya Mkoa wa Rukwa kutoa chanjo dhidi ya polio  Mganga Mkuu wa Serikali atafanya ziara katika Halmashauri ya Manispaa Sumbawanga ambapo atatembelea kituo Cha Afya Mazwi na Zahanati ya kilimahewa,pia atatembelea Halmashauri ya Wilaya Nkasi ambapo atatembelea hospitali ya Wilaya ya Nkasi na kituo Cha Afya Nkomolo. Profesa Nagu,amesisitiza kuwa watoto 391,883 walilengwa wapatiwe chanjo ili kuzuia maambukizi ya ugonjwa wa Polio ugonjwa huo ambao unaathiri watoto chini ya umri wa miaka 05 hadi 15.

MWENYEKITI WA CCM MKOA WA RUKWA AMPONGEZA MBUNGE KATIKA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM JIMBO LA KWELA.

Image
 Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Rukwa Bi.Sirafu Maufi apongeza taarifa ya tathimini ya utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ndani ya miaka mitatu ya Wilaya ya Sumbawanga vijijini iliyowasilishwa na Mbunge wa Jimbo la Kwela Mheshimiwa Deus Clement Sangu katika Mkutano wa Halmashauri kuu Wilayani humo. "Ninashukuru na kumpongeza Mbunge kwa kazi nzuri aliyoifanya ya utekelezaji wa Ilani ya Chama kwa kipindi Cha miaka mitatu iliyosimamiwa,kufuatiliwa na kutekeleza chini ya Uongozi wa Jimbo la Kwela ameonesha umahiri na uzalendo katika Jimbo lake la Kwela".Amesema Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Rukwa. Aidha Bi. Sirafu Maufi amewataka wanachama wa Chama Cha Mapinduzi Wilayani humo kuendelea kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan. Nae Mbunge wa Jimbo la Kwela Mheshimiwa Deus Sangu amesema kupitia fedha walizopata kutoka Serikali kuu wamefanikiwa kujenga kituo Cha Afya Kipeta na kupitia Mapato ya ndani ya Ha

WATOTO 391,883 KUPATIWA CHANJO YA POLIO RUKWA

Image
 Watoto 391,883 wenye umri chini ya miaka name wanatarajiwa kupatiwa chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa Polio. Kampeni hii ni maalumu kwa watoto waliozaliwa kuanzia mwaka 2016,Kampeni hii inakuja baada ya kuthibitika kwa kisa Cha Polio kwa mtoto Mmoja Manispaa ya Sumbawanga  Akifungua kikao Cha kamati ya Afya ya Mkoa kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Rukwa Mh.Lazaro Komba Mkuu wa wilaya Kalambo,amesema kuwa ugonjwa wa Polio unazuilika kwa kuwapatia chanjo watoto wote wenye umri chini ya miaka nane. Amewasisitiza kuwa wazazi na walezi kutoa taarifa katika vituo vya afya iwapo wataona dalili za watoto kupooza ghafla.Amehimiza jamii kuzingatia kanuni za Afya hasa kwa kunawa mikono kwa Maji safi yanayotiririka na kuagiza Kila kaya kuwa na choo Bora na kukitumia choo hicho ipasavyo ili kupunguza maambukizi ya magonjwa. Amewataka wazazi,walezi,viongozi wa dini na viongozi wa kimila kutoa ushirikiano kwa wataalamu wa Afya watakaokuwa wakitoa chanjo nyumba kwa nyumba,vituo vya Afya,katika mikusanyik

WANAFUNZI 7,522 WATARAJIA KUFANTA MTIHANI WA KUMALIZA DARASA LA SABA WILAYA YA KALAMBO

Image
 Mkuu wa wilaya Kalambo Mkoa wa Rukwa Lazaro Komba amesema wanafunzi 7,522 kati Yao wavulana wakiwa 3,404 na wasichana 4,118 wanatarajia kuanza kufanya mtihani wakumaliza Elimu ya msingi Wilayani Kalambo na kuwaonya vikali wasimamizi watakao bainika kuvujisha mitihani na kwamba Sheria Kali zitachukuliwa dhidi Yao. Aidha Komba amesema mitihani hiyo itafanyika kwenye vituo 330 kupitia shule 98 za Wilaya hiyo na Kila mkondo utakuwa na idadi ya watahiniwa 25 na kuwaonya vikali wazazi na walezi watakaobainika kujihusisha na tabia za kuwalaghai watoto wao kwa kuwazuia kufanya vizuri mitihani Yao kwa Nia ya kuwaozesha na kwamba Sheria Kali dhidi Yao zitachukuliwa. Hata hivyo kwa mujibu wa Afisa Elimu Mkoa wa Rukwa Samson Hango,amesema idadi ya watahiniwa kwa mwaka 2023 ni 32,217 ambapo imepungua kwa jumla ya watahiniwa 1,227 sawa na asilimia 3.8% ikilinganishwa na watahiniwa 33,444 waliosajiliwa mwaka 2022.

WAKULIMA NA WAFANYA BIASHARA KUJITANGAZA KITAIFA NA KIMATAIFA

Image
 Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Be.Gerlad Mweli ametoa wito wa wakulima na wadau wa kilimo kutumia Jukwaa la Mifumo ya Chakula Afrika 2023 (AGRF)katika kujitangaza  ili kuweza kunufaika na fursa za masoko ya ndani na nje ya nchi. Katibu Mkuu Mweli alikuwa anajibu swali lililoulizwa na miongoni mwa washiriki katika mkutano wa pembezoni mwa Jukwaa la Mifumo ya Chakula 2023 katika kikao Cha pamoja na Mawaziri na Makatibu wakuu kutoka Wizara za kilimo,Mifugo na uvuvi,Uchumi wa Buluu Zanzibar,kilimo ,ufugaji,umwagiliaji na italii Zanzibar pamoja na wadau wa kilimo. Bw.Mweli aliongeza na kusema kuwa wakulima watumie fursa mbalimbali za majadiliano yaliyoanza tarehe 5-8 Septemba 2023 ili kujifunza,kubadilishana  mawazo,kutangaza bidhaa na kuvutia italii na wawekezaji kwenye kilimo,na kutafuta masoko nje ya nchi. Wakulima na wafanya biashara wa mazao wamehamasishwa kutumia Jukwaa la kimtandao lijulikanalo Kama "M-kilimo"ambalo linawakutanisha wauzaji na wanunuzi kupata masoko kwa njia

SERIKALI KUANZA KUTUMIA MFUMO MPYA WA NEST KUFANYA MANUNUZI YA UMMA

Image
 Mafunzo rasmi ya siku Tano Leo,wataalamu kutoka Halmashauri za Mkoa wa Rukwa ya Mfumo mpya wa manunuzi wa umma kielektroniki NeST ili waweze kufanya manunuzi kupitia mfumo huo mpya ulioboreshwa zaidi. Akifungua mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa TEHAMA Mkoa wa Rukwa Katibu Tawala Msaidizi anayeshughulikia Masuala ya Utumishi na rasilimali watu Mkoa wa Rukwa Ndg.Donald Nssoko ambapo ameeleza kuwa Mafunzo hayo yatasaidia Usimamizi wa Sheria ya manunuzi, Kuongeza uwazi na kuzuia masuala ya Rushwa katika Mchakato wa manunuzi. Aidha amewataka Makatibu Tawala wasaidizi pamoja na wakuu wa vitengo ofisini hapo kuteua watumishi sahihi kutoka kwenye idara zote kama miongozo inavyoelekeza katika Matumizi sahihi ya Mfumo mpya wa NeST. Kwa upande wake Mkaguzi wa ndani Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa Ndg.Godfrey Haule amesisitiza kujenga umakini katika kutumia Mfumo huo mpya utakaosaidia kuepusha hoja zisizo nzuri za ukaguzi zinazojitokeza kutokana na Makosa ya kutumia Mfumo. Mafun

MPANGO WA UHAMASISHAJI WA USAJILI WATOTO CHINI YA MIAKA MITANO KUZINDULIWA

Image
 Wakala wa Usajili,ufilisi,na udhamini Nchini(RITA)unatarajia kuzindua mpango wa uhamasishaji wa usajili wa watoto chini ya miaka mitano ili waweze kupatiwa vyeti vya kuzaliwa. Hayo yamebainishwa kupitia Semina ya siku Moja iliyofanyika mkoani Kigoma ikihusisha viongozi waandamizi wa Serikali ikiwa ni pamoja na Katibu Tawala Mkoa,Makatibu Tawala Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri,Kamati ya Usalama Mkoa,Viongozi wa dini na wazee maarufu ili kuweza kutumia nafasi zao kuhamasisha jamii kushiriki kwenye zoezi Hilo. Naibu kadhi Wasii Mkuu Irene Lesulie amesema kuwa mpango huo unaolenga kusajili na kutoa vyeti kwa watoto wote wenye umri chini ya miaka mitano waliozaliwa Nchini kutokana na idadi ndogo ya watoto waliosajiliwa na kupata vyeti ikilinganishwa na idadi halisi ya waliozaliwa.