Posts

Showing posts from June, 2021

DK.MZINDAKAYA ALITOA MAELEKEZO HAYA AKIFA

Image
  Hayati Mpendwa mzee wetu Dk. Chrisant Mzindakaya mwanasiasa mkongwe nchini Tanzania aliyefariki katika hospitali ya Mhimbili jijini Dar es salaam alikokuwa akitibiwa anatajarajiwa kuzikwa Alhamisi Juni 12,2021 mida ya saa 9 Alasiri. Msemaji wa familia Frank Mzindakaya amesema Mzindakaya kabla hajafariki alitoa maelekezo ywa mahali pa kuzikiwa akifa.Hivyo familia itatekeleza jambo hilo.Hayati mzee wetu Dk. Mzindakaya anashikilia rekodi ya kuwa kiongozi aliyedumu katika uongozi kwa mda mrefu rekodi ambayo bado haijavunjwa na mtu yoyote hapa nchini kwa takribani miaka 40.Pumzika kwa amani mzee wetu tutaenzi mema na ushauri wako katika kulijenga Taifa letu la Tanzania.Imeandaliwa na Peter Helatano

NAMNA MRADI WA ELIMU JUMUISHI UNAVYOKUWA KWA JAMII

Image
  Mradi wa elimu jumuishi Sumbawanga umekuwa na matokeo chanya kwa jamii,wanajamii wamekuwa na uelewa mapana juu ya kuishi na watoto wenye mahitaji maalumu,namna ya kuwahudumia na kuzingatia miundombinu itakayokuwa rafiki kwa watoto wawapo nyumbani au shuleni pia. Lakini changamoto ni kwa baadhi ya shule kutotunza miundombinu inayoboreshwa na mradi huu. Hivyo sisi kama wanajamii tuamke na kuthamini msaada tunaopatiwa lakini pia kujitoa katika uchangiaji kwa watu wenye mahitaji maalumu. Mradi huu unalenga kuwasaidia watu wenye mahitaji maalumu ikiwa ni pamoja na kuwasaidia vifaa saidizi mradi ambao unasimamiwa na ERICK KAMKONO ambao unaratibiwa na kanisa la FPCT na ICD Kwa hapa Tanzania.  Imeandaliwa na Peter Helatano