Posts

Showing posts from October, 2023

WAZIRI MKUU ATIMIZA AHADI YAKE KWA REYO

Image
 Taasisi ya vijana inayojishughulisha na utunzaji wa Mazingira mkoani Rukwa(Rukwa Environmental Youth Organization-REYO)imekabidhiwa Pikipiki ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Majaliwa Kassim Majaliwa mapema mwaka huu alipofanya ziara katika Mkoa wa Rukwa. Amikabidhi Pikipiki hiyo kwa niaba ya Waziri Mkuu Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Charles Makongoro Nyerere ameishukuru ofisi ya Waziri Mkuu kwa kutimiza ahadi hiyo kwa Taasisi ya REYO. Ameipongeza Taasisi hiyo kwa kuendelea kutunza Mazingira na kuhamasisha wananchi kutunza Mazingira kwa kutokata miti na kuchoma moto hovyo misitu iliyopo. Akipokea Pikipiki hyo kwa niaba ya Taasisi ya REYO,Be.Issa Rubega amemshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa msaada huo ambao itasaidia kuendelea kampeni Ya utunzaji Mazingira kwa kuwa Pikipiki hiyo itasaidia kufika kwa urahisi na haraka katika maeneo yote.

ZIMAMOTO YATOA MAFUNZO KWA WATUMISHI RUKWA.

Image
 Jeshi la zimamoto Mkoani Rukwa limetoa mafunzo ya uokozi,kujikinga na kukabiliana na majanga ya moto kwa watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa. Mafunzo hayo yaliandaliwa na ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa kushirikiana na jeshi la zimamoto Mkoa wa Rukwa yakiwa na lengo la kuwapa watumishi wa umma ujuzi wa kuzuia,kuthibiti na kukabiliana vyema na majanga ya moto. Mafunzo hayo yalitofanyika oktoba 12,2023 yamehusisha utoaji wa Elimu juu ya hatua mbalimbali ya za kukabiliana na majanga ya moto,taratibu za uokoaji,na Matumizi sahihi ya vifaa vya kuzima moto na huduma ya kwanza. Akizungumza kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa,Bi .Sabina Msongela Kaimu Katibu Tawala utawala na usimamizi wa rasilimali watu Mkoa wa Rukwa amewashukuru watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa kushiriki mafunzo hayo.Amesema kuwa Mafunzo hayo yataongeza kujiamini kwa watumishi wa umma katika kuzuia na kuthibiti majanga ya moto. Jeshi la Zimamoto Mkoa wa Rukwa limeipongeza Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa kwa kuan