WATATU MBALONI UTAPELI KIMTANDAO

 

WATATU MBALONI UTAPELI KIMTANDAO

Jeshi la Polisi Mkoani Rukwa limewakamata wauhumiwa watatu(3)wanaume wakazi wa Sumbawanga amabo  wanaojihusisha na uhalifu wa kimtandao kwa njia ya kupiga simu na kuwatishia watu kwa nia ya kujipatia kipato.

Akitoa taarifa  Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Rukwa ACP- Shadrack Masija amesema wimbi la utapeli kupitia mtandao Mkoani Rukwa limekuwa likiongezeka na kusema kuwa Jeshi la Polisi linaendelea kujiimarisha na kuhakikisha wanatokomoeza utapeli wa kimtandao wa aina yotote ili kuhakikisha wananchi wanaishi kwa amani na utulivu.

Aidha Katika hatua nyingine Kamanda Masija amesema kumekuwepo na matukio mbalimbali ya watu kupoteza maisha kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha Katika Mkoa wa Rukwa mabapo Katika Wilaya ya Nkasi kumetokea vifo vya watu wawili akiwemo mwanafunzi mmoja na mvuvi mmoja,Wilaya ya kipolisi Laela kumetokea kifo cha mtu mmoja aliyetumbukia kwenye dimbwi lililojaa maji baada ya mvua kubwa kunyesha na kupelekea kifo chake.

Jeshi la Polisi linatoa wito kwa wananchi kuendelea kuota ushirikiano Katika kuripoti na kuzuia vitendo vya uhalifu au vinavyoweza kuhatarisha amani.


Comments

Popular posts from this blog

Watumishi Wa Umma Wilayani Kalambo Waungana Kuadhimisha Kumbukizi Ya Mashujaa Kwa Kufanya Usafi.

Dc Kalambo Ataka Walio Husika Kumuozesha Mwanafunzi Wa Darasa La Saba Kukamatwa

Mkurugenzi UTPC awataka Waandishi kuandika Habari za Usawa wa kijinsia ili kuleta mabadiliko Chanya katika jamii.