WANANCHI WATAKIWA KUPANDA MITI KUTUNZA MAZINGIRA.

 

WANANCHI WATAKIWA KUPANDA MITI KUTUNZA MAZINGIRA.

Wananchi mkoani Rukwa wametakiwa kuacha tabia ya kukata miti ovyo na kufanya shughuli za kilimo kwenye vyanzo vya maji

Hayo yamesemwa na mkuu wa mkoa wa Rukwa Queen Sendiga  alipotembelea ofisi ya klabu ya waandishi wa habari mkoani Rukwa na kuwataka  kufanya kazi kwa kuzingatia maadili ya kazi yao


Sendiga amesema anatarajia kupokea miche ya miti milioni moja ambayo tayari imeandaliwa na  Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) Mkoa wa Rukwa na itapandwa kwenye kingo za barabara na kwenye vyanzo vya maji.


Aidha amewataka watendaji wa kata na vijiji kwenye maeneo yao kuhakikisha wanasimamia zoezi la upandaji wa miti na utunzaji wa mazingira.

Katika hatua nyingine Sendiga amesema atahakikisha waandishi wa habari wanashirikiana na taasisi nyingine Katika kuutangaza Mkoa wa Rukwa na kutoa elimu ya utunzaji wa mazingira.



Comments

Popular posts from this blog

Watumishi Wa Umma Wilayani Kalambo Waungana Kuadhimisha Kumbukizi Ya Mashujaa Kwa Kufanya Usafi.

Dc Kalambo Ataka Walio Husika Kumuozesha Mwanafunzi Wa Darasa La Saba Kukamatwa

Mkurugenzi UTPC awataka Waandishi kuandika Habari za Usawa wa kijinsia ili kuleta mabadiliko Chanya katika jamii.