VIJANA WANATAKIWA KUTUMIA MITANDAO YA KIJAMII KUJIPATIA KIPATO.



 

NA: Franco NKYANDWALE SUMBAWANGA.            

VIJANA WANATAKIWA KUTUMIA MITANDAO YA KIJAMII KUJIPATIA KIPATO.

Vijana watakiwa kutumia mitandao ya kijamii kujiinua kiuchumi zama hizi za teknolojia na utandawazi badala ya kukaa vijiweni huku wakiilalamikia serikali kuwa hakuna ajira.

Hayo yameelezwa leo na Mhubiri Enala Malila wakati wa siku ya kuadhimisha sikukuu ya vijana kwenye Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Usharika wa Luther Dayosisi ya Ziwa Tanganyika katika Manispaa ya Sumbawanga.

“Wapo baadhi ya vijana ambao humiliki simu janja kubwa na zenye gharama ambazo huzitumia kuchati na kuangalia mambo ambayo huwapotosha kimamaadili, badala ya kuzifanya simu hizo kuwa mtaji ambapo wangewaza kutangaza biaashara zao ndogondogo wanazozifanya mitaani kwao,” Malila alifafanua.

Mzee wa Kanisa Mariamu Ndongokazialisoma somo la pili kutoka kwenye kitabu cha 1Timotheo 4:11-16, Mhubiri Malila alifafanua zaidi kuwa ili kijana aweze kufanikiwa kichumi ni lazima kijana aweze kujitambua, kukua kimwili, kiakili, kihisia, kiroho na kiuchumi kwa kumtegemea Mungu.

Mhubiri Malila aliwashauri vijana wenzake kuwa mitandao ya kijamii na simu janja ziwasaidie, kutafuta ajira, kujiendeleza kitaaluma, kutangaza Neno la Mungu kwa vitendo na vijana lazima wawe na uthubutu wenye utayari wa kufanya mambo yenye manufaa kwa jamii badala ya kuwa na maisha hatarishi na tegemezi.

Mwongoza ibada hiyo Upendo Msigwa alihitimishwa kwa kunukuu andiko la Biblia kutoka Mithali 4:10 alisema, vijana ni muhimu kuchagua mambo ya kufanya kutoka kwenye mitandao ya Kijamii na kufanya jambo kwa nia kulingana na mazingira walipo na si kwa ulegevu ila kwa bidii na uvumilivu ili kuepukana na umasikini wa kujitakia.

 

Comments

Popular posts from this blog

Watumishi Wa Umma Wilayani Kalambo Waungana Kuadhimisha Kumbukizi Ya Mashujaa Kwa Kufanya Usafi.

Dc Kalambo Ataka Walio Husika Kumuozesha Mwanafunzi Wa Darasa La Saba Kukamatwa

Mkurugenzi UTPC awataka Waandishi kuandika Habari za Usawa wa kijinsia ili kuleta mabadiliko Chanya katika jamii.