Kukumbatia ujuzi wa Dijitali mustakabali wa uandishi wa habari.


 

 

Kukumbatia  ujuzi wa Dijitali mustakabali wa uandishi wa habari.

Ulimwengu umeingia katika mfumo wa teknolojia iliyokuwa ,hivyo kupelekea kuachana na mfumo wa analojia na kwenda na dijital hii ina rahisisha namana nzuri ya mawasiliano,pamoja na upatikanaji wa taarifa  mbalimabali ndani na nje ya nchi,pia ni mabadiliko ambayo yanaendana  sambamba na ubunifu wa kidijital

Ujuzi wa kidigitali ni uwezo wa kutumia mbinu mpya za kiteknolojia katika kutatua matatizo ya kiutendaji katika  nafasi za uandishi wa habari na kupata matokeo chanya yanayomfanya kutambulika katika ulimwengu wa digitali.

Asha Abinallah ni kiongozi wa kampuni  ya media convergency inayotoa mafunzo kwa waandishi wa habari wanawake kuhusu uandishi wa kidigitali ikiwa na lengo la kuwaendeleza waandishi  wa habari katika uandishi wa habari kutumia teknolojia iliyokuwa.

Amesema  kupitia program hiyo maalumu ya mafunzo ya ujuzi kidigitali inawapa waandishi kupata uelewa na ujuzi wa namna ya kuandaa na kutengeneza maudhui kwa ajili  ya kuyatumia katika majukwaa ya kidijitali.

Abinallah ameongeza kuwa  kutumia  kutumia mitandao hiyo kama majukwaa ya uandishi wa habari kwa kuandaa vipindi,habari,makala wanavyoandaa  inasaidia kutengeneza fursa za kujiongezea kipato.

Lilian Urio ni mwandishi wa  kidigitali ambaye ni mkufunzi wa mafunzo ya uandishi wa kiditali,amesema  mwandishi  wa habari anapaswa  kujua stadi za kiditali ambazo ndio mwongozo katika kuandaa maudhui pamoja na kujua namna ya kutumia  majukwaa ya digitali.

,,ili kuweza kupata  habari na data kwa usahihi, ili kuandaa maudhui bora  nayanayoeleweka kwa jamii ni lazima wandishi ukubali kubadilika na uendane na kasi ya kukumbatia  huu ujuzi wa kidijitali,amesema Lilian Urio.

Naye peter Helatano mwandishi wa habari anaye wakilisha global tv online Mkoani Rukwa ,amesema ifike mahali waandishi wa habari waone umuhimu wa kukumbatia ujuzu huu wa dijitali kwa kuwa kunafursa nyingi  kwa mwanahabari ambazo zitawaongezea ujuzi,,amesema kupitia simu janja anayotumia inaweza kufanya vitu vingi sana amesema ndio ofisi yake  anayotumia kupata habari,na kutuma habari anazoandaa.

 

ANNA   MALISA

Comments

Popular posts from this blog

Watumishi Wa Umma Wilayani Kalambo Waungana Kuadhimisha Kumbukizi Ya Mashujaa Kwa Kufanya Usafi.

Dc Kalambo Ataka Walio Husika Kumuozesha Mwanafunzi Wa Darasa La Saba Kukamatwa

Mkurugenzi UTPC awataka Waandishi kuandika Habari za Usawa wa kijinsia ili kuleta mabadiliko Chanya katika jamii.