JIPANGENI ZAIDI KUHAKIKISHA WATU WANAJITOKEZA SIKU YA SENSA-ANNE MAKINDA-KAMISAA WA SENSA TANZANIA



 

Kamisaa wa sensa na Spika Mstaafu Anne Makinda amewataka viongozi wa mkoa wa Rukwa kujipanga kuhakikisha watu wengi zaidi wanajitokeza siku ya kuhesabiwa ifikapo Agosti 23 mwaka huu nchi itakapofanya zoezi la sensa ya watu na makazi.

 

Kiongozi huyo ametoa wito huo mjini Sumbawanga  wakati akizungumza na wadau kuhusu hali ya maandalizi ya sensa nchini pamoja na kutoa elimu ya umuhimu wa zoezi la sensa mwaka huu 2022.

 

Makinda alibainisha kuwa katika zoezi zoezi hili limejengwa katika msingi wa kiutawala ambapo utaratibu umewekwa  watu watahesabiwa pale alipolala.

 

" Tutahesabu watu wote mahala walipolala kama ni vituo vya mabasi, nyumba za wageni, katika kaya, waliopo hospitalini pia wale watakaokuwa kwenye magereza na mahabusu wote maharani wa sensa watawafikia kwa utaratibu uliowekwa na serikali" alisisitiza Mama Makinda.

 

Katika hatua nyingine Kamisaa huyo wa sensa alisema viongozi na jamii ya mkoa wa Rukwa ikumbuke umuhimu wa kutoa taarifa za walemavu Ili nao wahesabiwe kwenye sensa hatua itakayosaidia serikali kujua idadi yao na hali zao kuwezesha upatikanaji wa huduma stahiki.

 

Kamisaa huyo alishauri viongozi wa mkoa wa Rukwa kuendelea kutoa elimu kwa jamii juu ya zoezi hili ambapo ametaka wawaandae wananchi kushiriki ipasavyo katika kutoa majibu kwa maswali watakayoulizwa na makarani wa sensa Ikiwemo kuandaa vitambulisho au namba NIDA .

 

Naye Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti alisema kwa juwamkoa huo upo mpakani tayari vyombo ya dola vimejiandaa kushirikiana na wataalam  kufanikisha zoezi la sensa ili raia wanaostahili kuhesabiwa wajItokeze huku ulinzi ukiimarishwa.

 

"Sensa ni takwa la kisheria tutasimamia vema,licha ya mkoa wetu kuwa mpakani tumejipanga kusimamia zoezi hili kwa kutumia vyombo vyetu ya ulinzi na usalama " alisisitiza Mkirikiti. 

 

Mkirikiti alitoa rai kwa vyombo vya habari hususan radio za kijamii zikizopo mkoa wa Rukwa kutoa nafsi kwa wataalam  wa sensa na viongozi kutoa elimu na hamasa juu ya sensa ya watu na makazi ili wananfhi wengi wapate uelewana hatumaye wajitokeze siku ya kuhesabiwa.

 

Akitoa taarifa kuhusu maandalizi ya sensa ngazi mkoa,Mratibu wa mkoa Adam Ramadhan alisema tayari vituo vya kuhesabia watu 2,190 vimeandaliwa kwenye halmashauri  nne za Sumbawanga  Manispaa, Sumbawanga vijijini,Nkasi na Kalambo.

 

Kamisaa wa Sensa ya Watu na Makazi Mama Anne Makinda anendelea na ziara yaje ya kutoa elimu na hamasa ya sensa ambapo leo pia atazungumza kwenye mkutano wa hadhara kiiji cha Kasanga wilaya ya Kalambo.

Comments

Popular posts from this blog

Watumishi Wa Umma Wilayani Kalambo Waungana Kuadhimisha Kumbukizi Ya Mashujaa Kwa Kufanya Usafi.

Dc Kalambo Ataka Walio Husika Kumuozesha Mwanafunzi Wa Darasa La Saba Kukamatwa

Mkurugenzi UTPC awataka Waandishi kuandika Habari za Usawa wa kijinsia ili kuleta mabadiliko Chanya katika jamii.