WATOTO 124,498 KUSAJILIWA KUPATA CHETI CHA KUZALIWA RUKWA



 

Na Peter Helatano

Mkoa wa Rukwa umefanikiwa kusajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto 124,498 chini ya mpango wa Usajili wa watoto walio na umri chini ya miaka mitano unaoratibiwa na Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA) ulioanza Novemba mwaka 2021 .

Mafanikio hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti  wakati akifungua kikao cha tathmini kuhusu utekelezaji wa mpango huo kilichofanyika mjini Sumbawanga.

Kwa upande wake Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA) Charles Salyeem alisema Mpango huo umeleta maboresho makubwa katika mfumo wa usajili wa vizazi na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto kwani sasa huduma hiyo inapatikana katika Ofisi za Watendaji Kata na Vituo vya Tiba kote mkoani  Rukwa.

.

Zoezi hili la usajili wa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto chini ya umri wa miaka mitano linaendelea nchini na hakuna malipo yoyote hivyo ni wazi wanajamii kujitokeza na kuwapeleka watoto kuwasajili.

 

MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

Watumishi Wa Umma Wilayani Kalambo Waungana Kuadhimisha Kumbukizi Ya Mashujaa Kwa Kufanya Usafi.

Dc Kalambo Ataka Walio Husika Kumuozesha Mwanafunzi Wa Darasa La Saba Kukamatwa

Mkurugenzi UTPC awataka Waandishi kuandika Habari za Usawa wa kijinsia ili kuleta mabadiliko Chanya katika jamii.