Watumishi wa Umma wilayani Kalambo mkoani Rukwa wameungana na watu wengine katika kuadhimisha siku ya kumbukumbu ya mashujaa kwa kufanya usafi kwenye majengo ya hospitali ya wilaya hiyo ili kuendeleza kampeni ya usafi wilayani humo. Zoezi hilo liliongozwa na Mkuu wa wilaya hiyo Lazaro Komba alisisitiza kuwa zoezi hilo ni endelevu kwa kila siku ya mwisho wa mwezi ili kukabiliana na magonjwa ya milipuko ikiwemo kipindupindu na magonjwa ya kuhara. Komba alisisitiza wananchi kujenga mazoea kufanya usafi wa mazingira kuzunguma maeneo yao husika kwa lengo la kuifanya wilaya kuwa safi muda na wakati wote. ‘’Kimsingi leo tumekutana kufanya usafi hapa kwenye majengo ya Hospitali ya wilaya Kalambo kama sehemu ya kuadhimisha kumbukizi ya siku ya mashujaa na maadhimisho haya kwa ngazi ya kitaifa yanafainyika mkoani Dodoma’’ alisema komba. Mapema akiongea na Watumishi wa umma wakati wa shughuli za usafi kwenye maeneo hayo ,Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo Shafi Mpenda alisema
Mkuu wa wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa Lazaro Komba ameliagiza Jeshi la polisi wilayani humo kuwakamata wazazi na walezi waliomwozesha mwanafunzi wa darasa la saba katika shule ya msingi Mbuza kata ya Mkowe mwenye umri wa miaka 17 na kumuozesha kwa Asulwa Sikombe mkazi wa kijiji cha Mbuza. Taarifa kutoka kwa kwenye uongozi wa kijiji hicho akiwemo mwenyekiti wa kijiji hicho Alisen Machenchelwa na mkuu wa shule hiyo Fedelisi Mbuluko zimeeleza kuwa mwanafunzi huyo Mach 2023 alitoroka kwenye makazi ya wazazi wake na kutokomea kusiko fahamika na kwamba baada ya kurejea June 2023 wazazi wake walimua kumuozesha kwa ndugu Asulwa Sikombe mkazi wa kijiji cha Mbuza. Walieleza kuwa baada ya kupata taarifa hizo waliamua kuwakamata wazazi wa binti huyo na kuwafikisha kwenye kituo cha polisi Matai kwa hatua zaidi. Hata hivyo mapema akiongea ofisini kwake mkuu wa wilaya hiyo Lazaro Komba amesema mpaka sasa Jeshi la polisi linamsaka aliyeozeshwa mwanafunzi huyo na kwamba wazazi wawili wa mwanafun
Na.Neema Mtuka Mkurugenzi Mtendaji wa Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania(UTPC) Bw.Kenneth Simbaya amewataka Waandishi wa Habari kuendelea kuandika Habari za Usawa wa kijinsia ili kuleta mabadiliko Chanya kwa jamii. Simbaya ameyasema hayo wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo Waandishi wa Habari za Usawa wa kijinsia yaliyo wakutanisha Waandishi wa Tanzania Bara na visiwani. Ameongeza kuwa Waandishi wanapaswa kuibua Habari za ukatili wa kijinsia ambazo zitasaidia jamii kubadili mitazamo hasi na kuachana na Mila potofu zilizopitwa na wakati ambazo Bado Zina mkandamiza mwanamke na kupotea maana ya Usawa wa kijinsia Aidha amesema Waandishi wa Habari washirikiane kwa pamoja katika kuibua mambo mbalimbali yahusuyo jamii na kufanya kazi kwa pamoja na kuhakikisha wanazingatia maadili ya uandishi wa Habari kanuni na taratibu zilizopo. Mafunzo ya Usawa wa kijinsia yanafanyika mjini Morogoro ambapo pamoja na mambo mengine Waandishi wanatazamia kuleta mabadiliko makubwa katika jam
Comments
Post a Comment