MWONGOZO WA KUPAMBANA NA RUSHWA KWA VIJANA WA SKAUTI RUKWA

 


MWONGOZO WA KUPAMBANA NA RUSHWA KWA VIJANA WA SKAUTI RUKWA 

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Joseph Mkirikiti leo amekabidhiwa mwongozo wa kupambana na rushwa kwa vijana wa skauti mkoa wa Rukwa kwenye hafla iliyofanyika kwenye viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa mjini Sumbawanga. 

Akikabidhi Mwongozo huo ,Kamanda wa TAKUKURU  Mkoa wa Rukwa Bw. Daniel  Ntera  alisema lengo la serikali ni kuona vijana wakifundishwa njia mbalimbali za kukabiliana na rushwa wakiwa mashuleni. 

Mwongozo huo utatumika kwa vijana wa skauti kuanzia shule za msingi, sekondari hadi vyuo ambapo pia walimu watatumika kufundishia elimu ya kudhibiti na kupambana na rushwa kwenye jamii ya watanzania.

Comments

Popular posts from this blog

Watumishi Wa Umma Wilayani Kalambo Waungana Kuadhimisha Kumbukizi Ya Mashujaa Kwa Kufanya Usafi.

Dc Kalambo Ataka Walio Husika Kumuozesha Mwanafunzi Wa Darasa La Saba Kukamatwa

Mkurugenzi UTPC awataka Waandishi kuandika Habari za Usawa wa kijinsia ili kuleta mabadiliko Chanya katika jamii.