Jeshi la Polisi mkoani Rukwa linawashikilia watu watatu wote wakazi wa Kirando wilayani Nkasi kwa tuhuma ya kufukua kaburi la marehemu asiyefahamika jina lake na kukata kichwa chake kisha kwenda kukitelekeza kwenye kichanja cha kuanikia vyombo nje ya nyumba ya mkazi mmoja wa kijiji cha Kirando Mkoani Rukwa. Regina Samwel katika maelezo yake anadai aliamka kwenda uani lakini anakutana na harufu kali isiyoyakawaida hivyo alirudi ndani kumwarifu mamake aliyetoka nje na kukuta kichwa cha binadamu kimehifadhiwa kwenye sufuria juu ya kichanja cha vyombo kilichopo nje ya nymba yao. Katika uchunguzi wa awali wa Polisi katika eneo la Kirando walifanikiwa kumkamata mtu mmoja kutokana na mfanano wa nyayo zake zilizoonekana kwenye eneo la tukio na hata kwenye kaburi hilo, hali iliyowashangaza hata wakazi wa eneo hilo wakidai kuwa hawajawahi ona tukio la aina hiyo maisha mwao. Kamanda wa Polisi mkoani Rukwa William Mwampaghale amesema licha ya ku...
Being,China -Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU)inashiriki kongamano la 5 la kimataifa la mashirikiano katika mapambano dhidi ya rushwa,linaloendelea jijini Beijing China. Kongamano hili limewakutanisha mamlaka 219 kutoka nchi 121 duniani,likilenga kubafilishana uzoefu na utaalamu katika jukumu la kuzuia na kupambana na rushwa Kongamano hili la siku Tano limejumuisha warsha ya viongozi wa mamlaka za kuzuia na kupambana na rushwa(high level Forum),ambapo Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU ,Bw.Crispin Francis Chalamila,amewasilisha mada kuhusu "mfumo wa Sheria wa Tanzania katika mapambano dhidi ya rushwa"katika mada yake Bw.Chalamila ameeleza jinsi ambavyo serikali ya Tanzania imekuwa ikijipambanua katika mapambano dhidi ya rushwa kwa kuimarisha mifumo ya Sheria na ya kitaasisi.Alibainisha uanzishwaji wa divisheni ya mahakama kuu inayoshughulikia masuala ya rushwa na uhujumu uchumi kuwa ni hatua muhimu katika kuhakikisha uwajibikaji na utawala Bora. TAKUKURU...
RC SENDIGA: TUTAFANYA MAPINDUZI YA KILIMO RUKWA Na. OMM Rukwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Queen Sendiga amesema anatamani kuona mkoa wa Rukwa ukifanya mapinduzi makubwa katika sekta ya kilimo kiwe cha kibiashara na kukuza uchumi wa wananchi. Ili kufanikisha hilo amewataka wataalam wa kilimo katika halmashauri zote nne za Rukwa kuja na mikakati ya kufanya kilimo kichangie zaidi katika kukuza pato la wananchi na kuongeza uhakika wa chakula. Mkuu huyo wa Mkoa amesema hayo jana mjini Sumbawanga (10 Agosti, 2022) wakati wa hafla rasmi ya makabidhiano ya ofisi toka kwa mtangulizi wake Joseph Mkirikiti kufuatia Rais Samia Suluhu Hassan kumteua kuwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa. “Natamani kuiona Rukwa ikifanya mapinduzi makubwa katika kilimo. Maafisa kilimo na ugani jitahidini kuwa na mipango mizuri ili kilimo chetu kiwe cha kibiashara na kuhusisha vijana wengi “alisema Sendiga. Sendiga aliongeza kusema mkoa lazima uwe na mkakati wa kufanya vijana wengi kurudi vijijini ili kufanya ...
Comments
Post a Comment