SERIKALI KUWEKA MIPAKA KULINDA VYANZO VYA MAJI Serikali Wilayani Nkasi Mkoani Rukwa imeanza Uwekaji wa mipaka kati ya Pori la Akiba Lwafi na Kijiji cha Mtogolo kilichopo Wilayani Nkasi Mkoani Rukwa ili Kulinda chanzo cha maji katika bwawa la Mfili amabalo ni tegemeo la maji Katika Wilaya ya Nkasi kutokana na bwawa hilo kukausha maji kutokana na shuguli za kibinadamu zinazodaiwa kufanyika pembezoni mwa bwawa hilo. Hayo yamejiri Katika zoezi la uhuishaji wa hifadhi ya msitu wa Lwafi ambopo Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Peter Lijualikali amewataka wananchi kuzingatia maelekezo ya Serikali ili kulinda vyanzo vya maji Wananchi Katika maeneo hayo wanadai kuishi mda mrefu huku kilio chao ni kuhakikisha wanapatiwa maeneo mengine kama walivyoahidiwa na Serikali
Karibu Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote Wapendwa watanzania wenzangu, Ili kufanikisha dira yetu ya: “Kufanikisha upatikanaji wa huduma za mawasiliano Tanzania kikamilifu na kwa usawa”, Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) unalenga kuimarisha uwezo wa kushirikiana na watoa huduma za mawasiliano nchini ili kuhakikisha ufikiaji wa huduma za mawasiliano katika maeneo yote yenye mawasiliano hafifu pamoja na yale yasiyo na huduma hiyo kabisa. Katika kutekeleza majukumu yake, Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) umejielekeza katika kubaini maeneo ya miradi ya mawasiliano ambayo yanaweza kupata ruzuku Serikalini kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote, lengo ni kuhakikisha wananchi wote wanafikiwa na huduma za mawasiliano ambayo kwa kiasi kikubwa yanachangia katika uchumi wa mwananchi mmoja mmoja na Serikali kwa ujumla. Tangu kuanza kazi kwa Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF) mwaka 2009, kumekuwa na mafanikio mengi katika sekta ya mawasiliano, ...
Being,China -Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU)inashiriki kongamano la 5 la kimataifa la mashirikiano katika mapambano dhidi ya rushwa,linaloendelea jijini Beijing China. Kongamano hili limewakutanisha mamlaka 219 kutoka nchi 121 duniani,likilenga kubafilishana uzoefu na utaalamu katika jukumu la kuzuia na kupambana na rushwa Kongamano hili la siku Tano limejumuisha warsha ya viongozi wa mamlaka za kuzuia na kupambana na rushwa(high level Forum),ambapo Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU ,Bw.Crispin Francis Chalamila,amewasilisha mada kuhusu "mfumo wa Sheria wa Tanzania katika mapambano dhidi ya rushwa"katika mada yake Bw.Chalamila ameeleza jinsi ambavyo serikali ya Tanzania imekuwa ikijipambanua katika mapambano dhidi ya rushwa kwa kuimarisha mifumo ya Sheria na ya kitaasisi.Alibainisha uanzishwaji wa divisheni ya mahakama kuu inayoshughulikia masuala ya rushwa na uhujumu uchumi kuwa ni hatua muhimu katika kuhakikisha uwajibikaji na utawala Bora. TAKUKURU...
Comments
Post a Comment