MAFUNZO YA KUONGEZA UELEWA NA KUPUNGUZA UNYANYAPAA KWA JAMII NA WAHUDUMU WA AFYA KATIKA UTOAJI WA HUDUMA ZA AFYA WA WATU WENYE ULEMAVU.

 







.Shilikisho la vyama vya watu wenye ulemavu Tanzania [ SHIVYAWATA] Wameiomba  serikali kuwepo haja ya kutoa elimu kwa watoa huduma za Afya ili kuwahudumia kwa ustadi watu wenye ulemavu. Huduma za Afya kwa watu wenye ulemavu nchini Tanzania bado zinakabiliwa na changamoto licha ya sera na sheria za nchi kusema kuwa kundi hili lipatiwe bure matibabu ikiwemo kupewa kipaumbele. Baadhi ya changamoto wanazokutana nazo watu wenye ulemavu katika kupata huduma za afya ni pamoja na;

       Miundo mbinu isiyo rafiki katika vituo vya kutolea huduma za afya mfano; vyoo, njia maalumu kwa ajili ya walemavu. Pia baadhi ya watu wenye ulemavu kukosa vifaa saidizi kama vile wheel chairs hivyo kuwa hatarini kupata maambukizi ya magonjwa wanapokuwa katika vituo vya kupatia huduma za afya

       Lugha (Mawasiliano) hasa kwa watu wenye ulemavu wa kusikia (uziwi)na kutoongea hivyo kupelekea changamoto katika kuwasiliana na watoa huduma kwani wengi hawajui lugha ya alama. Pia elimu ya afya inayotolewa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya kutowafikia ipasavyo watu wenye ulemevu mfano watu wenye ulemavu wa kuona

Comments

Popular posts from this blog

Watumishi Wa Umma Wilayani Kalambo Waungana Kuadhimisha Kumbukizi Ya Mashujaa Kwa Kufanya Usafi.

Dc Kalambo Ataka Walio Husika Kumuozesha Mwanafunzi Wa Darasa La Saba Kukamatwa

Mkurugenzi UTPC awataka Waandishi kuandika Habari za Usawa wa kijinsia ili kuleta mabadiliko Chanya katika jamii.