Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo ametoa maagizo kwa Manispaa ya Sumbawanga kukamilisha ujenzi wa shule ya msingi Mkuyuni ili kuepusha mlundikano na wanafunzi kutembea umbali kwenda shule ya Msingi King'ombe.
Watumishi Wa Umma Wilayani Kalambo Waungana Kuadhimisha Kumbukizi Ya Mashujaa Kwa Kufanya Usafi.
Watumishi wa Umma wilayani Kalambo mkoani Rukwa wameungana na watu wengine katika kuadhimisha siku ya kumbukumbu ya mashujaa kwa kufanya usafi kwenye majengo ya hospitali ya wilaya hiyo ili kuendeleza kampeni ya usafi wilayani humo. Zoezi hilo liliongozwa na Mkuu wa wilaya hiyo Lazaro Komba alisisitiza kuwa zoezi hilo ni endelevu kwa kila siku ya mwisho wa mwezi ili kukabiliana na magonjwa ya milipuko ikiwemo kipindupindu na magonjwa ya kuhara. Komba alisisitiza wananchi kujenga mazoea kufanya usafi wa mazingira kuzunguma maeneo yao husika kwa lengo la kuifanya wilaya kuwa safi muda na wakati wote. ‘’Kimsingi leo tumekutana kufanya usafi hapa kwenye majengo ya Hospitali ya wilaya Kalambo kama sehemu ya kuadhimisha kumbukizi ya siku ya mashujaa na maadhimisho haya kwa ngazi ya kitaifa yanafainyika mkoani Dodoma’’ alisema komba. Mapema akiongea na Watumishi wa umma wakati wa shughuli za usafi kwenye maeneo hayo ,Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo Shafi Mpenda alisema
Comments
Post a Comment