Maelfu Ya Waumini Wajitokeza Kuombea Uchaguzi''kalambo.''



Na Baraka Lusajo. Rukwa

Waamini pamoja  na wachungaji kutoka  madhehebu mbalimbali  ya  dini kwa kushirikiana na kamati ya ulinzi na usalama wilayani  Kalambo mkoani Rukwa, wameungana kuendesha  kongamano la  kumuomba mwenyezi Mungu ili uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu, uwe wa haki  ili kuilinda amani na utulivu uliopo kwa lengo la  kuivusha nchi ikiwa salama bila  kumwaga damu.


Makamu askofu wa kanisa la FPCT jimbo la  Rukwa na katavi Andrea  Mwakalinga  amesema  watumishi  wa  Mungu  tunahitaji kamapeni safi bila  ugomvi  na kwamba kufanya fujo  ni  kukosa hekima  ya  kimungu.

Amesema  kwa kuwa  wagombea  wote wanatoka  katika makanisa na misikiti  yetu, Mashehe na Wachungaji tuta hakikisha tuna hubiri amani na utulivu kwenye mihadhara  yetu.

‘’sisi tuna watu wengi wanao tufuata makanisani na misikitini mwetu, hivyo hatunabudi kuhimiza upendo ili zifanyike kamapeni zisizo na ugonvi kwenye majukwaa ya siasa. Na ijulikane kuwa mtu yeyote atakaye fanya kampeni za fujo kuelekea uchaguzi huu, atakuwa hana nia njema katika ustawi wa nchi yetu.’’ Amesema mwakalinga.


Shehe  wa  wilaya  hiyo Sulemani Amani, alisema  kila  mtu  amefika  katika  eneo  hilo kwa  lengo la kufanya maombi na kuwataka  washirika wote kuomba  katika  roho na kweli ili kuhakikisha maombi hayo yanafika kwa mwenyezi mungu kama  ilivyo kusudiwa.


Mkuu wa wilaya ya Kalambo Calorius Misungwi, amesema kila mwananchi  anatakiwa kuchagua  viongozi bora baada ya kusikiliza sera  zao.

‘’Sisi kazi  yetu kama  wananchi ni kusikiliza sera na kuchagua viongozi wenye sifa  safi. Hivyo wote tuhamasike na tujitokeze kwa  wingi  kuchagua  viongozi bora  ambao  watakuwa  msaada  kwa  wilaya na taifa  kwa  ujumla.’’ Amesisitiza Misungwi.

 

 

 

Comments

Popular posts from this blog

UTPC KUENDELEA KUELIMISHA UMMA,UMUHIMU WA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI

WALIOFUKUA KABURI WAKAMATWA NA JESHI LA POLISI RUKWA