Posts

Showing posts from August, 2024

CHONGOLO AIPONGEZA HALMASHAURI YA KALAMBO KUANZISHA TEKNOLOJIA MPYA YA UKAUSHAJI WA DAGAA NA SAMAKI

Image
 Na Neema Mtuka. Mkuu wa mkoa Songwe Mhe.Daniel Chongoro ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa kwa kuanzisha teknolojia mpya ya UKAUSHAJI wa DAGAA na SAMAKI kwa kutumia kaushio la kisasa (Solar tent drier)ambalo litawezesha upatikanaji wa samaki na dagaa wenye ubora na kuwezesha wavuvi kujikwamua na Hali ya kiuchumi. Ameyasema hao baada ya kutembelea Banda la Halmashauri ya Wilaya Kalambo kupitia maonesho ya wakulima nanenane yanayofanyika kikanda jijini Mbeya na kuipongeza Halmashauri ya Wilaya Kalambo kwa kuanzisha teknolojia hiyo ambayo itawezesha kupunguza upotevu wa mazao ya uvuvi baada ya kuvuliwa hususani kipindi Cha masika. Awali akitoa taarifa kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa wilaya hiyo Shafi Mpenda ,Afisa uvuvi Wilayani humo Bw.Abdul Balozi,Amesema sambamba na teknolojia hiyo pia wameleta bidhaa mpya ya unga wa samaki ambayo ni ya kwanza kwa Kanda ya nyanda za juu kusini ambayo itasaidia  kupunguza udumavu na utapiamlo kwa watoto kutokana na unga huo k

BALOZI WA SWEDEN NCHINI ATEMBELEA KLABU YA WAANDISHI WA HABARI KILIMANJARO

Image
  Mwandishi wetu Jana Agosti 5,2024 Balozi wa Sweden nchini Tanzania Mh.Charlotta Ozaki Macias ametembelea klabu ya waandishi wa Habari Kilimanjaro (MECKI) kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na klabu hiyo pamoja na kufanya mazungumzo na wanachama wa klabu hiyo. Mh.Balozi pia ametaka kujua mchango wa MECKI kwa jamii katika kupaza sauti Ili kuibua Changamoto zilizopo kwenye jamii na namna klabu hiyo ilivyojipanga kuelekea uchaguzi wa Serikali za mitaa na uchaguzi Mkuu 2025. Pamoja na mambo mengine Mh.Balozi na wanachama hao wamejadiliana masuala mbalimbali ikiwemo uhuru wa Vyombo vya Habari na namna ya kuandika Habari za uchunguzi. Aidha Mh. Charlotta ameambatana na timu kutoka Muungano wa klabu za waandishi wa Habari Tanzania (UTPC)iliyokuwa ikiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji Kenneth Simbaya.